Wednesday 10 April 2013

Historia ya Wanyambo

Wanyambo ni kabila lilokuwa miongoni mwa makabila makubwa na yenye nguvu za kivita na kiuchumi.Watu wa kabila hili la wanyambo walikuwa na ufalme ulioongozwa na wafalme Abakama 14 kwa nyakati tofauti.Watu wake ni wakulima na wafugaji. Historia ya kabila hili ilifahamika ukanda wote wa Ziwa Magharibi Victoria pamoja na nchi za Rwanda na Burundi.Kutokana na uhunzi wa mapambo mengi ya kifalme yalitengenezwa na kuhifadhiwa kwenye ngome ya mfalme.Mapambo hayo yalipendwa na mengine yalichukuliwa na Wajerumani ,walipewa zawadi na Omukama Rumanyika. Kwa ujumla ni kabila lililoheshimika hivyo wanyambo walijivunia Unyambo wao hali iliyoibua misemo kama, Ndyu Munyambo akala nakalenje, Omunyambo agamba echabweine. Aidha anasema siku ya utamaduni wa Mtanzania ni utaratibu uliobuniwa na Bodi ya Makumbusho ya Taifa chini ya Wizara ya Elimu na Utamaduni mwaka 1994 kabla Makumbusho ya taifa haijahamishwa chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kama ilivyo sasa ili kutoa fursa kwa jamii mbalimbali hapa nchini kuonyesha tamaduni zao katika Kijiji cha Makumbusho ,Kijitonyama,Dar es Salaam.

Nyumba za kiasili za wanyambo 

Wanyambo wengi hawajitambui

Inasemekana kwamba hata wanyambo wenyewe hasa waishio nje ya Karagwe hawana ufahamu kama wao ni wanyambo au ni wahaya kwa sababu baadhi yao hujitambulisha kama ni wahaya na wanajaribu hata kuigiza lugha yao. Historia ya Wanyambo haijatafitiwa kwa kina na hivyo hakuna machapisho ya kutosha yanayoelezea historia ya Wanyambo.Yapo machapisho machache sana hasa ya Profesa Katoke na hadithi za wapelelezi kana Hans Mayer ambayo hayako sokoni tena na yaliyopo hayatoshelezi mahitaji. Anasema mila na desturi za Wanyambo zilizo nje ziko hatarini kutoweka ikiwa ni pamoja na ngoma za asili, nyimbo ,misemo ,majigambo,hadithi na taratibu za maisha nyingi zimetoweka na zilizobaki ziko hatarini kupotea kabisa. Mfano mzuri ni ngoma ya Amakondere ambayo imebaki ikichezwa na kundi moja tu la wazee waishio Rwanyango ambazo hazijarekodiwa ambapo itakuwa vigumu kurithishwa kizazi kimoja hadi kingine. Aidha uwepo wa ngoma ile unategemea sana uhai wa wazee hao hata ala za muziki wa ngoma hizo (Amakondere) hazilimwi tena na huenda mmea huu umeshatoweka kabisa.Kwa upande wa lugha ya wanyambo (Orunyambo) imeanza kupoteza uhalisia wake kutokana na mwingiliano na kutozungumzwa mara kwa mara hivyo huenda ikapotea kabisa. “Kwa ujumla wanyambo wanapata usumbufu katika kujitambulisha hasa wanapohitaji baadhi ya huduma katika Wizara ya Mambo ya Ndani kwa sababu hudhaniwa jamii ya wanyambo ni wakimbizi kutoka nchi jirani za Burundi na Rwanda”.

1 comment:

  1. hivi ndivyo tunaweza kutambulisha na kuendeleza kabila letu siyo kuwasindikiza wenzetu.pamoja tunaweza

    ReplyDelete